Sowah Atangaza Vita Kuwania Kiatu Cha Dhahabu Ligi Kuu NBC
Mshambuliaji mpya wa Singida Black Stars, Jonathan Sowah, ameweka wazi dhamira yake ya kutikisa Ligi Kuu Tanzania Bara kwa ushindani mkali katika mbio za kuwania Kiatu cha Dhahabu msimu wa 2024/2025. Nyota huyo raia wa Ghana amekuwa kwenye kiwango bora tangu ajiunge na Singida Black Stars, akionesha uwezo wa hali ya juu katika safu ya ushambuliaji.
Sowah alijiunga na Singida Black Stars katika dirisha dogo la usajili la Januari 2024 akitokea Al-Nasr Benghazi ya Libya, timu aliyoitumikia kwa miezi sita. Akiwa na kikosi hicho cha Libya, alihusika katika mabao saba kwa kufunga matano na kutoa pasi mbili za mabao katika mechi tisa.
Kabla ya kuhamia Al-Nasr Benghazi, Sowah alikuwa akikipiga katika klabu ya Medeama ya Ghana, ambako alionesha kiwango cha juu kwa kufunga mabao 16 katika mechi 20 za Ligi Kuu ya Ghana.Mshambuliaji mpya wa Singida Black Stars, Jonathan Sowah |
Katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika, Sowah alifunga mabao matatu katika mechi saba, jambo lililozifanya klabu mbalimbali kuvutiwa naye, ikiwemo Yanga SC, baada ya kuonesha makali yake dhidi ya miamba hiyo ya Tanzania. Aidha, mchango wake ulisaidia Medeama kutwaa taji la FA nchini Ghana, huku akitwaa tuzo ya Mchezaji Bora wa Mwaka wa timu hiyo na kuorodheshwa kwenye kikosi cha mwisho cha Ghana kilichoshiriki AFCON 2023.
Mafanikio Yake na Singida Black Stars
Tangu ajiunga na Singida Black Stars, Sowah amecheza mechi sita za
Ligi Kuu Tanzania Bara na kufunga mabao saba, ikiwa ni wastani wa bao
moja kila mchezo. Uwezo wake wa kufumania nyavu umechangia kuleta
ushindani mkali katika vita ya ufungaji bora, huku akizidiwa mabao manne
na vinara wa orodha hiyo—Jean Charles Ahoua wa Simba SC, Prince Dube na
Clement Mzize wa Yanga SC, ambao wana mabao 10 kila mmoja.
READ ALSO:
- Wafungaji Bora NBC Premier League 2024-2025
- NBC Premier League Statistics 2024/2025: Top Scorers, Top Assist and Top Clean Sheets
- YANGA SC Watamba Tuzo za Februari Ligi Kuu ya NBC 2024/25
- Msimamo wa Ligi Kuu Tanzania 2024/2025 - NBC Premier League Table 2024/2025
- Wafungaji Bora Ligi Kuu ya Wanawake Tanzania (TWPL) 2024/2025
- Bado Nina Wasiwasi na SIMBA Mbele ya Al Masry
- Exclusive: Aliyoongea Mwakinyo Baada ya Polisi Kumuachia
- Wapinzani wa Simba Robo Fainali Kombe la Shirikisho CAF 2024/25
- CAF: Vikosi Bora Ligi ya Mabingwa Afrika na Kombe la Shirikisho Afrika 2024/25
- ORODHA ya Vilabu Bora Afrika 2025 (CAF Club Ranking 2025)
- YANGA WAKIKAZA HAPA WATAMPOTEZA MAZIMA SIMBA CAF
- Timu Zinazoshiriki African Football League AFL 2024/2025 | CAF Super League
- Ratiba ya Ligi Kuu Tanzania Bara 2024-2025 | NBC Premier League Fixtures 2024-2025
- Timu Tajiri Zaidi Tanzania 2023/24 - Richest Football Teams Tanzania
- Mshahara Wa Clatous Chota Chama Yanga 2024/2025
- Mshahara Wa Stephane Aziz Ki Yanga 2024-2025
- Wasifu/CV ya Joshua Mutale Winga Mpya wa Simba 2024/25
- Wasifu/CV Ya Steven Mukwala Mchezaji Mpya Wa Simba 2024/2025
- CV ya Ahoua Jean Charles Mchezaji Mpya Wa Simba SC 2024/2025
- CV ya Boka Chadrak Beki Mpya Wa Yanga 2024/2025 Hii Hapa
- CV ya Duke Abuya Mchezaji Mpya wa Yanga 2024
- Who Will Lead Zinedine Zidane?
- Jezi 10 Bora za Timu za Afrika
- Team 50 Bora Africa: CAF Ranking of African Clubs Men’s
- Wafungaji Bora | Top Scorers CAF Champions League
- Ligi 10 Bora Dunian | FIFA Ranking
- Zawadi za Washindi – CAF Champions League 2024/2025
- Top 10 ya Viungo (Midfielders) Bora Duniani
- Washindi Wote Tuzo za CAF 2023 – Full List CAF Awards Winners 2023
- Ijue Simba Historia ya Simba SC
- Mishahara ya Wachezaji | Simba SC Players Salaries
- CV ya Ladaki Chasambi Mchezaji Mpya wa Simba 2024
- Soweto Derby History – Top Derby in Africa
- The History and Achievements of Mamelodi Sundowns F.C
Kaimu kocha mkuu wa Singida Black Stars, David Ouma, ameeleza kuwa ujio wa Sowah umeongeza morali kwa washambuliaji wengine wa timu hiyo, hali inayoboresha ushindani ndani ya kikosi. “Malengo yetu ni kumaliza nafasi nne za juu, na hilo linawezekana iwapo kila mchezaji ataendelea kupambana. Sowah ni mshambuliaji mzuri na mchango wake kwa timu ni wa thamani kubwa,” alisema Ouma.
Sowah Azungumzia Malengo Yake
Akizungumzia ushindani wa Kiatu cha Dhahabu, Sowah amesema hana muda wa kupoteza na dhamira yake ni kuhakikisha anakuwa miongoni mwa wafungaji bora wa ligi. “Nilipofika Tanzania, nilitazama msimamo wa wafungaji na nikamwona Elvis Rupia akiwa kinara. Sasa Jean Charles Ahoua wa Simba anaongoza, lakini mimi sijaja kuwa mshabiki, nimekuja kupambana,” alisema mshambuliaji huyo mwenye ari kubwa.
Kwa sasa, msimamo wa wafungaji unaongozwa na Jean Charles Ahoua mwenye mabao 12, akifuatiwa na Clement Mzize na Prince Dube wa Yanga wenye mabao 10 kila mmoja. Steven Mukwala wa Simba na Elvis Rupia wanashikilia nafasi ya tatu wakiwa na mabao tisa, huku Leonel Ateba (Simba) na Peter Lwasa wakiwa na mabao nane. Sowah, pamoja na Stephane Aziz Ki wa Yanga, wanashikilia nafasi ya tano kwa mabao saba kila mmoja.
No comments:
Post a Comment